Ripoti ya KNCHR kuhusu maandamano
0
0
05/07/24
Watu 361 walijeruhiwa, 627 walikamatwa na 32 hawajulikani waliko kufuatia maandamano ya kupinga mswada wa fedha. hiyo ni kwa mujibu wa tume ya kutetea haki za binadamu nchini. Tume hiyo imekashifu vikali vurugu zilizoshuhudiwa wakati wa maandamano hayo ambayo wahalifu wa kukodiwa walishiriki na kusababisha maafisa wa usalama kutumia nguvu kupita kiasi. sasa tume imetaka serikali ikumbatie mzungumzo ili kutafuta suluhu ya haraka.
Montre plus
0 commentaires
sort Trier par